Skip to main content

Featured

Maombolezo: Hii ndiyo Hali Ilivyo Tanzania Bendera Yapepea Nusu Mringoti

Agizo la Rais John Magufuli la Bendera ya Taifa kupepea kwa nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia leo Septemba 22 kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere iliyotokea mkoani Mwanza limetekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Wanaoingiza zana haramu wakabwa koo

Serikali imetakiwa kuongeza juhudi katika kupambana na wafanyabiashara wanaoingiza na kutengeneza zana haramu za Uvuvi badala ya kutumia nguvu nyingi kuziteketeza zana hizo kutoka kwa wavuvi.
Akizungumza mjini hapa leo Januari 28  na wanachama wa umoja wa vijana we Chama Chama Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Mara, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa, Kheri James amesema  umoja huo unaungana na serikali katika kupigwa vita uvuvi haramu lakini unapingana na mbinu zinazotumika.
Amesema  katika zoezi linaloendelea hasa katika mikoa ya kanda ya ziwa badala ya kusaidia watumishi wa serikali wanaotekeleza zoezi hilo wamekuwa wakichonganisha wananchi na rais John Magufuli.
“Juhudi zinazotumika katika kuchoma zana hizo zinatakiwa kutumika  kuhakikisha zana hizo haziingii nchini kupitia mipaka yote na wala kutengenezwa na kuwepo katika masoko ya ndani ya nchi,” alisema James
Amesema Serikali inatakiwa kujiuliza ni kwani ni zana hizo haramu zimezagaa katika soko la ndani na hatimaye kutumiwa  na wavuvi wengi ambapo amesema kuwa kukosekana kwa nyavu halali kunaweza kusababishwa na sababu nyingi ikiwemo bei kubwa kutokana na ushuru wa nyavu hizo pamoja na malighafi zake kuwa juu.
“Tusikubali operesheni chonganishi ikiendeshwa kwa kisingizo cha kusimamia sheria, umemkamata mtu na nyavu haramu ukazichoma, ukamtoza faini ya Sh20 milioni akalipa, bado unamchomea mtumbwi wake na kumnyanga'nya samaki hivi huku ni kusimamia sheria au kumkomoa mwanachi wa kawaida," amesisitiza mwenyekiti huyo
James amesema kuwa haiwezekani serikali ikawaona watumiaji wa nyavu hizo na kushindwa kujua ni akina nani wanaziingiza katika soko la Tanzania aidha kupitia mipakani au kutoka katika viwanda vilivyopo nchini na kuzitaka mamlaka husika kuhakikisha kuwa wote wanaojihusisha na biashara ya kutengeneza na kukuza zana hizo wanakamatwa na kuchukuliwa hatua kali.
Amesema “iweleweke wazi kuwa sisi UVCCM hautuungi mkono Uvuvi haramu ila tunapinga mbinu zinazotumika maana zinalenga kumkomoa mnyonge sasa tunawataka wahusika waongeze juhudi kuhakikisha kuwa wale wanaosababisha zana hizo kuwepo wanashughulikiwa kwa mujibu wa sheria,”
Mmoja wa vijana wa chama hicho wilayani hapaThomas John amesema vijana wengi wamekosa ajira na wengine kuamua kujiajiri huku akiomba wapewe mitaji ili waweze kujiajiri vijana wengi.

Comments

Popular Posts