Skip to main content

Featured

Maombolezo: Hii ndiyo Hali Ilivyo Tanzania Bendera Yapepea Nusu Mringoti

Agizo la Rais John Magufuli la Bendera ya Taifa kupepea kwa nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia leo Septemba 22 kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere iliyotokea mkoani Mwanza limetekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Lukuvi atoa agizo kwa taasisi za Serikali

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amezitaka wizara, taasisi za Serikali na vyombo vyote vya umma kupima maeneo yao na kuyawekea alama za mipaka kuepusha uvamizi.
Lukuvi amesema hayo baada ya kukagua maeneo yenye migogoro ya ardhi katika Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.
Akiambata na naibu wake, Angelina Mabula ambaye ni mbunge wa Ilemela, Lukuvi ametembelea maeneo yaliyovamiwa na wananchi ya Polisi Kigoto-Kirumba, Uwanja wa Ndege wa Mwanza na eneo la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) la Nyamirolerwa.
Katika taarifa ya wizara iliyotolewa leo Jumapili Januari 28,2018 Lukuvi amezitaka taasisi zote za Serikali kupima maeneo yao ili wananchi wayatambue.
Amewataka waliojenga ndani ya hifadhi ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuondoa maendelezo yao ndani ya siku saba kabla ya kuchukuliwa hatua.
Lukuvi amesema hawaruhusiwi kukaa karibu na eneo linalorusha na kutua vyombo vya anga jambo ambalo ni hatari kwao na usalama wa vyombo hivyo.
Pia, amezitaka halmashauri zote nchini kukamilisha ukusanyaji wa kodi ya ardhi kabla ya Aprili 30.
Ametoa agizo hilo baada ya kukutana na watumishi na wakuu wa idara wa Manispaa ya Ilemela na wa Jiji la Mwanza baada ya kukagua mifumo ya ulipaji kodi ya pango la ardhi na maendeleo ya urasimishaji makazi mkoani Mwanza.
Mwisho.

Comments

Popular Posts