Skip to main content

Featured

Maombolezo: Hii ndiyo Hali Ilivyo Tanzania Bendera Yapepea Nusu Mringoti

Agizo la Rais John Magufuli la Bendera ya Taifa kupepea kwa nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia leo Septemba 22 kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere iliyotokea mkoani Mwanza limetekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Chadema wasitisha Kampeni kushiriki mazishi ya Kingunge

Mwenyekiti wa Chadema  Freeman Mbowe ametangaza kusitishwa  kwa kampeni ili kujumuika katika mazishi ya Kingunge Ngombale Mwiru.
Hayo aliyasema  kwenye kampeni za kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni Salum Mwalimu kwenye viwanja vya Kinondoni manyanya.
Mbowe alisema Kingunge ni mtu alifanya mengi kwenye taifa hili kutokana na uadilifu wake na kesho kwa pamoja tunamsindikiza.
"Mzee Kingunge ni mtu mwadilifu amefanya mengi kwenye taifa hili alikuwa CCM na baadaye Chadema kesho tutasitisha kampeni ili kushiriki maziko" amesema Mbowe.
Naye  mgombea ubunge  Mwalimu amesema vipaumbele vyake ni vitatu ila atakapochaguliwa ataanza na elimu pamoja na afya.
"Najua kata nyingi hazina vituo vya afya wala shule za kata mtakaponichagua kipaumbele changu cha kwanza nitahakikisha  kila kata inakuwa na kituo cha afya na shule ya sekondari" alisema Mwalimu.

Comments