Skip to main content

Featured

Maombolezo: Hii ndiyo Hali Ilivyo Tanzania Bendera Yapepea Nusu Mringoti

Agizo la Rais John Magufuli la Bendera ya Taifa kupepea kwa nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia leo Septemba 22 kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere iliyotokea mkoani Mwanza limetekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Ukarabati MV Mapinduzi wagharimu Sh300 mil



Zanzibar. Zaidi ya Sh300 milioni, zimetumika hadi sasa katika ukarabati wa meli ya MV Mapinduzi (11) kutokana na hitilafu zilizosababisha meli hiyo kutofanya kazi kwa zaidi ya miezi mitatu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Miundo Mbinu, Mustafa Aboud Jumbe alitaka kiwango hicho cha fedha juzi wakati alipotembelea meli hiyo katika Bandari ya Malindi mjini Unguja.
“Tumetumia kiwango hicho kutokana na kununua vifaa vipya kutoka Uholanzi, fedha zinaweza kuongezeka kwani kuna ukarabati zaidi,” alisema Jumbe.
Alifafanua kuwa kwa sasa tayari baadhi ya vifaa hivyo vimeanza kufungwa na mafundi wataalamu kutoka Uholanzi wakishirikiana na mafundi wazawa waliopo Zanzibar.
Akizungumzia kuhusu sababu za kuharibika kwa mashine hiyo, alisema wanaendelea na uchunguzi ili kubaini sababu zilizosababisha kuharibika kwa kwake. “Nataka niweke wazi, hakuna mtu aliyehusika kuharibu mashine hii isipokuwa ni hitilafu, tunafanya uchunguzi kujua hitilafu hizo zilisababishwa na nini,” alisema Jumbe.
Kapteni mkuu wa meli hiyo, Aboubakar Mzee Ali alisema harakati za ufungaji wa vifaa kwenye mashine ya meli hiyo unaendelea vizuri na kuahidi ndani ya siku 10 zijazo watakuwa wamekamilisha.

Comments

Popular Posts