Katibu Tawala mpya wa Mkoa wa Songwe, David Kafulila
Dar es Salaam. Katibu Tawala mpya wa Mkoa wa Songwe, David Kafulila amejikuta akila kiapo mara mbili baada ya kukosea kusimama, leo Agosti 1 Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kafulila, aliyewahi kuwa mbunge wa Kasulu, (NCCR-Mageuzi) aliteuliwa na Rais John Magufuli wiki iliyopita.
Kafulila alionekana kusimama akiwa ameelekea upande wa kushoto na ndipo alipoelekezwa kumwelekea Rais.
Katibu Mkuu kiongozi, John Kijazi alipoona kasoro hiyo, alimwelekeza Kafulika kumwelekea Rais na akaapa upya.
Mbali na Kafulila, Jill Maleko Katibu tawala mkoa wa Mtwara naye alitakiwa kurudia kiapo chake.
Comments
Post a Comment