Skip to main content

Featured

Maombolezo: Hii ndiyo Hali Ilivyo Tanzania Bendera Yapepea Nusu Mringoti

Agizo la Rais John Magufuli la Bendera ya Taifa kupepea kwa nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia leo Septemba 22 kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere iliyotokea mkoani Mwanza limetekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Updates: Waliofariki Kivuko cha MV Nyerere Wafika 148


Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na ajali ya Kivuko cha MV. Nyerere kilichozama katika eneo la Bwisya, takribani mita 100 kabla ya kufika bandari ya Ukara imefikia 148, huku kazi ya ukoaji likiendelea.

Kivuko hicho kinachofanya safari kwa kusafirisha abiria na mizigo kati ya Ukara na Bugorora wilayani Ukerewe, kilizama juzi majira ya saa 8:10 mchana baada ya kutoka katika bandari ya Bugorora kwenda Ukara.

Kutokana na ajali hiyo, watu 40 pekee ndio waliookolewa wakiwa hai na 136 waliopolewa wakiwa wameshafariki dunia hadi jana jioni.

Leo Septemba 22, 2018 asubuhi Miili mingine 12 imeopolewa  na hivyo kufanya miili iliyopatikana hadi sasa kufikia 148.

Comments

Popular Posts